Quran Apps in many lanuages:

Surah Ash-Shu'ara Ayahs #120 Translated in Swahili

قَالُوا لَئِنْ لَمْ تَنْتَهِ يَا نُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِي وَمَنْ مَعِيَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.
فَأَنْجَيْنَاهُ وَمَنْ مَعَهُ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.
ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ الْبَاقِينَ
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.

Choose other languages: