Quran Apps in many lanuages:

Surah Nooh Ayahs #9 Translated in Swahili

قَالَ رَبِّ إِنِّي دَعَوْتُ قَوْمِي لَيْلًا وَنَهَارًا
Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,
فَلَمْ يَزِدْهُمْ دُعَائِي إِلَّا فِرَارًا
Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.
وَإِنِّي كُلَّمَا دَعَوْتُهُمْ لِتَغْفِرَ لَهُمْ جَعَلُوا أَصَابِعَهُمْ فِي آذَانِهِمْ وَاسْتَغْشَوْا ثِيَابَهُمْ وَأَصَرُّوا وَاسْتَكْبَرُوا اسْتِكْبَارًا
Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!
ثُمَّ إِنِّي دَعَوْتُهُمْ جِهَارًا
Tena niliwaita kwa uwazi,
ثُمَّ إِنِّي أَعْلَنْتُ لَهُمْ وَأَسْرَرْتُ لَهُمْ إِسْرَارًا
Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.

Choose other languages: