Quran Apps in many lanuages:

Surah Ash-Shu'ara Ayahs #118 Translated in Swahili

وَمَا أَنَا بِطَارِدِ الْمُؤْمِنِينَ
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُبِينٌ
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
قَالُوا لَئِنْ لَمْ تَنْتَهِ يَا نُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِي وَمَنْ مَعِيَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.

Choose other languages: