Quran Apps in many lanuages:

Surah Maryam Ayahs #81 Translated in Swahili

أَفَرَأَيْتَ الَّذِي كَفَرَ بِآيَاتِنَا وَقَالَ لَأُوتَيَنَّ مَالًا وَوَلَدًا
Je, umemwona aliye zikanya Ishara zetu na akasema: Kwa hakika mimi nitapewa mali na wana!
أَطَّلَعَ الْغَيْبَ أَمِ اتَّخَذَ عِنْدَ الرَّحْمَٰنِ عَهْدًا
Kwani yeye amepata khabari za ghaibu, au amechukua ahadi kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema?
كَلَّا ۚ سَنَكْتُبُ مَا يَقُولُ وَنَمُدُّ لَهُ مِنَ الْعَذَابِ مَدًّا
Hasha! Tutaandika anayo yasema, tutamkunjulia muda wa adhabu.
وَنَرِثُهُ مَا يَقُولُ وَيَأْتِينَا فَرْدًا
Na tutamrithi hayo anayo yasema, na atatufikia mtupu peke yake!
وَاتَّخَذُوا مِنْ دُونِ اللَّهِ آلِهَةً لِيَكُونُوا لَهُمْ عِزًّا
Na wamechukua miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati iwape nguvu.

Choose other languages: