Quran Apps in many lanuages:

Surah Ash-Shu'ara Ayahs #155 Translated in Swahili

وَلَا تُطِيعُوا أَمْرَ الْمُسْرِفِينَ
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,
الَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.
قَالُوا إِنَّمَا أَنْتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.
مَا أَنْتَ إِلَّا بَشَرٌ مِثْلُنَا فَأْتِ بِآيَةٍ إِنْ كُنْتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
قَالَ هَٰذِهِ نَاقَةٌ لَهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَعْلُومٍ
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.

Choose other languages: