Quran Apps in many lanuages:

Surah Al-Mumenoon Ayahs #106 Translated in Swahili

فَمَنْ ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ
Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa.
وَمَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَٰئِكَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنْفُسَهُمْ فِي جَهَنَّمَ خَالِدُونَ
Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia khasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu.
تَلْفَحُ وُجُوهَهُمُ النَّارُ وَهُمْ فِيهَا كَالِحُونَ
Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizo kunjana.
أَلَمْ تَكُنْ آيَاتِي تُتْلَىٰ عَلَيْكُمْ فَكُنْتُمْ بِهَا تُكَذِّبُونَ
Je! Hazikuwa Aya zangu mkisomewa, na nyinyi mkizikanusha?
قَالُوا رَبَّنَا غَلَبَتْ عَلَيْنَا شِقْوَتُنَا وَكُنَّا قَوْمًا ضَالِّينَ
Mola wetu Mlezi! Tulizidiwa na uovu wetu na tukawa watu tulio potea.

Choose other languages: