Quran Apps in many lanuages:

Surah Al-Hijr Ayahs #82 Translated in Swahili

وَإِنْ كَانَ أَصْحَابُ الْأَيْكَةِ لَظَالِمِينَ
Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
فَانْتَقَمْنَا مِنْهُمْ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٍ مُبِينٍ
Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
وَلَقَدْ كَذَّبَ أَصْحَابُ الْحِجْرِ الْمُرْسَلِينَ
Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.
وَآتَيْنَاهُمْ آيَاتِنَا فَكَانُوا عَنْهَا مُعْرِضِينَ
Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.
وَكَانُوا يَنْحِتُونَ مِنَ الْجِبَالِ بُيُوتًا آمِنِينَ
Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.

Choose other languages: